Kunihusu

Picha yangu
Teacher, comedian and event master of ceremonies.

Alhamisi, 27 Aprili 2017

TAZAMA ROBOTI INAYOWEZA KUPAMBANA NA WAHALIFU.





Ubunifu ndio unaiendesha dunia lakini sio kila mtu amepewa uwezo wa kubuni bali wapo wachache kwenye kundi la wengi ambao wana uwezo wa kubuni mambo mbalimbali ndiyo maana nimekuletea stori hii ya ubunifu wa hali ya juu.

Kampuni ya Silicon Valley imebuni mbinu mpya ya kupambana na uhalifu katika maduka makubwa baada ya kutengeneza robot ambayo kazi yake ni kupambana na uhalifu katika maduka makubwa zikitengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu ambapo zitafanya kazi bila usimamizi wa binadam na kukodishwa kwa Dollar 7 (£5) ambazo ni sawa Tsh. 15,400 kwa saa.

Katika stori hii iliyochapishwa na mtandao wa Daily Mail April 27, 2017 ni kwamba robot inayoitwa Knightscope K5 ina urefu wa futi 5 ni maalum kufanya patrol katika maduka makubwa, viwanja vya michezo na kumbi za cinema kwa lengo la kuhakikisha usalama wa maeneo hayo.

Lengo kuu la kampuni hiyo ni kuzalisha maroboti wengi zaidi ambao watasambazwa duniani kote wakikusudia kupunguza uhalifu hadi 50% ambapo kwa mujibu wa ripoti ni kuwa wanakusudia siku moja zitumike na Polisi katika kusaidia kupambana na uhalifu.

Mmoja wa watengenezaji wa Knightscope Stacy Dean Stephens alisema: “Tunaanza na maeneo ya umma, hivyo tunaziruhusu kufanya patrol kwenye maeneo kama maduka makubwa, kampasi, viwanja vya michezo na nyumba za cinema.”

Jumatatu, 17 Aprili 2017

MAGAZETI  YA LEO TAREHE 18 Aprili  2017















Source: Millardayo.com

L

RAIS MAGUFULI AITAKA TCU IWAACHIE WANAFUNZI WACHAGUE VYUO WANAVYOVITAKA.

Rais John Magufuli ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kutowachagulia vyuo wanafunzi wa elimu ya juu na kuwaacha wanafunzi hao kuchagua vyuo wanavyovitaka wenyewe.




Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Rais Magufuli alipokuwa akizindua mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambapo alikitaka chuo hicho pia kutoza Sh 500 kwa siku tofauti na Sh 800 ambazo zinatoswa kwa hosteli nyingine.

“Ninaamini kama wanafunzi wangepewa nafasi ya kuchagua vyuo wanavyovipenda wenyewe, vyuo vya Serikali kama vile Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kikuu cha Mzumbe vingekuwa na wanafunzi wengi sana,” alisema Magufuli.

Aliendelea kwa kusema kuwa TCU imekuwa ikiwachagulia wanafunzi vyuo visivyo na sifa na makazi ya wanafunzi hivyo kusababisha wanafunzi hao kusoma katika mazingira magumu na wanapomaliza masomo yao hukosa ajira kutokana na vyuo hivyo kutokuwa na sifa. Rais Magufuli alitaka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) lenyewe kubaki na udhibiti.

Aidha alisema ni vyema Tume ikabaki na majukumu yake kama kuhimiza ubadilishaji wa maarifa/elimu kwa njia ya kuunganisha kimtandao Vyuo Vikuu na Vyuo vya Vyuo Vikuu, usajili na utambuzi rasmi wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Vyuo Vikuu, uthibitishaji wa programu za kitaaluma, uthibitishaji na uratibu wa udahili wa wanafunzi.

Majukumu mengine ni ufuatiliaji na udhibiti wa elimu bora Vyuo Vikuu na Vyuo vya Vyuo Vikuu, ukusanyaji na usambazaji wa taarifa/ data kuhusu elimu ya juu. “Niombe tu kwa Wizara ya Elimu na TCU tubadilishe kidogo utaratibu wa kuchagulia wanafunzi, wanafunzi wawe wanachagua vyuo badala ya TCU kuwachagulia vyuo vya kwenda,” alisema. Akifafanua zaidi alisema kama wanafunzi wakijichaguliwa vyuo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kingejaa wanafunzi 23,000 wanaotakiwa kuwepo katika chuo hicho.

“Lakini sijajua ni kwa nini mtu amefaulu anataka kuja hapa afaidi mabweni ya Magufuli analazimishwa kwenda kwenye kachuo ambako hakana jina akasome pale, wakati hakuna hata mabweni, saa nyingine hata walimu hawana, tunawatesa watoto hawa,” alisema. Alisema anafahamu ingawa hana ushahidi kuwa wakuu wa vyuo hivyo wanatoa fedha kwa viongozi wa TCU ili wapangiwe idadi ya wanafunzi wanaowahitaji kwenye vyuo vyao.

Rais Magufuli alisema kuwa TCU ibaki kuwa mdhibiti wa elimu lakini wanafunzi wabaki kuwa na haki ya kuchagua vyuo kwani baadhi ya vyuo vinaendesha shughuli zake kwa mikopo ya wanafunzi hao. “Tuwaache watoto wachague vyuo wanavyovitaka, vile ambavyo havitachaguliwa, vife kwanini mnalazimisha vyuo ambavyo havina ubora vipate wanafunzi msipolazimisha vyuo ambavyo vina ubora vitapata watu….. najua maneno haya hayawafurahishi baadhi ya watu na mimi siko hapa kumfurahisha mtu?” alisema Rais Magufuli.

Chanzo: bongo5.com

MKE WA ROMA ATOA YAKE YA MOYONI KUHUSU KUTEKWA KWA MUMEWE.


Mke wa msanii Roma Mkatoliki, Nancy Mshana amefunguka kwa mara ya kwanza toka mume wake alipotekwa na kupatikana na kuwashukuru Watanzania ambao walikuwa pamoja na yeye katika kipindi kigumu.
Roma akiwa na mtoto wake.

Mrembo huyo ametumia maneno ya kwenye Biblia kutoka katika kitabu cha Yeremia kufikisha ujumbe wake kwa watu ambao wamemfanyia ubaya mume wake na kusema kuwa na wao watakutwa na mabaya hayo.

“(Yeremia 30:16-17) Basi, watu wote wakulao wataliwa; na adui zako wote watakwenda kufungwa; kila mmoja wao; na hao waliokuteka nyara watatekwa; na wote waliokuwinda nitawafanya kuwa mawindo. Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana.Ameen” Alinukuu mke wa Roma Mkatoliki.

Mbali na hilo Nancy alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wote ambao wamesimama na wao katika kipindi hiki kigumu.

“Ahsanteni wote mliosimama na sisi katika kipindi kigumu tulichopitia !! Mungu awabariki sana” aliandika Nancy.

Msanii Roma Mkatoliki bado anaendelea na matibabu kufuatia tukio lake la kutekwa na kuumizwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

Alhamisi, 13 Aprili 2017

MWENGE  WA UHURU WIZI MTUPU.

MWENGE wa uhuru umezinduliwa hivi karibuni na Samia Suluhu, Makamu wa Rais katika viwanja vya Jamhuri Mkoani Morogoro. Mwenge huo “utakimbizwa” nchi nzima.
Mwenge huo kwetu utapita, kwenu umepita au bado? Kama bado basi unakuja. Bahati mbaya tu kwamba kwa mara ya kwanza tangu niwe na akili timamu nilihudhuria mbio za Mwenge mwaka 2011 kwetu Singida.
Niliyoyaona yalinifanya niwalaumu watu wote wakubwa kuliko mimi, ambao kila siku wamevumilia mambo ya hovyo yanayofanywa kwa kivuli cha mbio za Mwenge wa Uhuru.
Ilikuwa ni bahati ya pekee kwa viongozi wa serikali kushindwa kufikiri, hadi wakaamua kunialika nihudhurie katika mbio za Mwenge wa Uhuru. Huko nilijifunza mengi.
Watakaokasirika kwa kusoma haya, wajue lengo langu limefanikiwa, kwani sikuwa na lengo la kuwafurahisha tangu nilipofikiria kuandika haya kuhusu Mwenge.
Upuuzi huu unaanzia katika gharama za kukimbiza Mwenge. Msafara huu unahusisha mkuu wa mkoa, wilaya na sekretarieti zote, usalama wa taifa, Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU), Uhamiaji, Polisi, Jeshi, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wananchi.
Katika hiyo orodha ndefu, watu wote wanalipwa pesa, tangu mkubwa mpaka mdogo, hadi waandishi wa habari. Pesa inayotumika kwa shughuli ya Mwenge ni nyingi. Msafara wa Mwenge unahusisha magari mengi, yanayojazwa mafuta. Magari mengi yenye namba za PT, STK, STL, STJ, RC na magari ya mwenyekiti na katibu wa CCM, pia yapo mengine yenye namba binafsi.
Nikiwa katika Shule ya Msingi Lusilile, ambako yalifanyika mabidhiano kati ya Mkoa wa Singida na Dodoma, niliona takribani magari 120 au zaidi, kwa misafara yote miwili iliyokutana hapo.
Kimsingi, Mwenge unatumia gharama kubwa mno, kiasi kwamba fedha hizo zingetumika kufanya shughuli za maendeleo, baadhi ya kero kwa wananchi ama zingekwisha au kupungua kwa kiasi kikubwa.
Inashangaza kuona kuwa Mwenge ule ulikabidhiwa katika eneo la shule ambayo haikuwa na madawati.
Njia nzima katika Wilaya ya Manyoni, Singida, tangu tumepokea Mwenge, shule zote njiani wanafunzi walikuwa wamejipanga barabarani, hawakusoma siku hiyo. Lakini hata Mwenge haukusimama njiani.
Wananchi wa Lusilile na vijiji jirani waliniambia kuwa kulikuwa na msako maalumu kwa wananchi watakaokiuka kuhudhuria mbio za Mwenge, hivyo walilazimika kujipanga barabarani tangu asubuhi na baadaye kupigwa na jua kali, njaa na kiu zao hadi Mwenge ulipopita.
Wapo waliolazimishwa kucheza ngoma ili ionekane wanaufurahia Mwenge. Kifupi, wapo wananchi ambao hawakufanya kazi za kujiingizia kipato ili kuheshimu amri ya kuhudhuria mbio za Mwenge
Hata hivyo, katika mbio za Mwenge, Mwenyekiti wa CCM na katibu wake, pamoja na viongozi wa Umoja wa vijana wa chama hicho  (UVCCM)  ni watu wa kuheshimiwa kuliko hata askari wa cheo cha juu.
Kuna bajeti ya kuweka mafuta gari ya Mwenyekiti wa CCM, Katibu wa CCM,  wa UWT, na UVCCM, japo wanahadaa kuwa Mwenge ni wa kitaifa. Ni uongo, kuthibitisha hili, huwezi kuona popote risiti ya mafuta kwa magari ya wenyeviti wa mikoa wa TLP, NCCR, CUF, CHADEMA, NLD.
Kichefuchefu kingine ni kwamba kuna fungu la kununua nguo za mapokezi ya Mwenge, zipo tofauti kati ya  ofisi ya mkuu wa mkoa, ofisi ya katibu tawala wa mkoa, ofisi ya mkuu wa wilaya Ofisi ya TAKUKURU, ofisi ya Usalama wa Taifa na viongozi wengine.
Pia unakuta kuna sare za mapokezi ya Mwenge zingine za kimbizia Mwenge.  Fungu la suti hizo zilitosha kununua madawati kwa ajili ya darasa moja la shule waliyoenda kukabidhiana Mwenge ambayo haikuwa na madawati.
Mwenge unatembezwa na kaulimbiu za “kumulika wezi na wala rushwa,” nilishtuka zaidi tulipokuwa Manyoni Mjini, ukarabati wa mnara wa Mwenge, mnara ambao umejengwa miaka mingi huko nyuma, mnara ulipigwa rangi na kuandikwa kaulimbiu ya “Tumethubutu, tumeweza, na Tunasonga mbele” kwa gharama ya Sh. 2.5 milioni. Haiingii akilini. Watanzania tuache kuhalalisha wizi wa kimachomacho kama huu.
Mwenge ni nini? Kwanini unatumika kama alama katika mavazi na kadi za UVCCM? Mwenge una msafara mrefu kuliko hata msafara wa rais?
Katika msafara 


JESHI LA POLISI LATOA TAHADHARI KWENYE MSIMU HUU WA PASAKA.


Jashi la polisi nchini limetoa tahadhari kwa wananchi kuelekea msimu huu wa Sikuu ya Pasaka kuhusiana na suala zima la ulinzi na usalama wa mali zao huku likisema kuwa kuna baadhi ya watu hutumia sikukuu hizi kufanya vitendo vya uhalifu hasa wizi wa kutumia silaha, wizi wa magari, utapeli na vitendo vingine.

Taarifa ndiyo hii hapa chini

RAIS MAGUFULI AMPIGIA SIMU MWANA FA


Jioni ya April 12 2017 staa wa muziki wa hip hop bongo Hamisi Mwinjuma ambaye wengi tunamfahamu kwa jina la Mwana FA, alitoa taarifa kupitia ukurasa wake wa twitter kuoneshwa kufurahisha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kumpigia simu.

Mwana FA ambaye kwa sasa anafanya vizuri katika radio na tv stations mbambali kwa hit single yake ya Dume Suruali amethibitisha kupigiwa simu na Rais kumwambi anakubali kazi zake.



Kupitia ukurasa rasmi wa twitter wa staa huyo uliyokuwa verified aliandika “nimefurahi kupokea simu ya Mheshimiwa Rais @MagufuliJP kunisalimia na kuniambia yeye ni mpenzi wa kazi zangu,haswa #DumeSuruali..”

Jumatano, 12 Aprili 2017

MAGAZETI YA LEO TAREHE 13 Aprili 2017

























MWAKYEMBE AELEZA SABABU ZA KUWEPO KWENYE  MKUTANO WA ROMA.


Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia, Jumanne hii alipata nafasi ya kusimama bungeni Dodoma ambapo alielezea kushangazwa na kitendo cha Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe kuwepo kwenye mkutano wa waandishi wa habari na rapper Roma aliyetekwa hivi karibuni na watu wasiojulikana.




Hatimaye Dkt Mwakyembe, Jumatano hii amesimama bungeni kujibu hoja hiyo.

“Nianze na suala la kwanza ambalo ni la uelewa ambalo mheshimiwa Nkamia alionyesha mshangao hapa kuniona mimi niko na msanii Roma Mkatoliki anayedaiwa kutekwa na wenzie watatu siku chache zilizopita. Mheshimiwa mwenyekiti wakati namsikiliza Nkamia jijini Dar es Salaam nilikuwa na kundi kubwa la waandishi wa habari na wao walikuwa wanamshangaa kwanini anashangaa nikiwa kiongozi kwenye idara hii anaelewa kuwa idara ya habari maelezo ni wizara ya habari,utamaduni, sanaa na michezo, kwahiyo ni ofisi yangu ile, na hivi karibuni tumehamia Dodoma Makao makuu yapo pale LAPF. Nikiwa Dar es Salaam ofisi yangu ipo Maelezo kwahiyo mtu akinikuta maelezo mimi ndiyo nimemfuata yeye au yeye ndiyo kanifuata? Sasa ni vitu ambavyo vinatakiwa vieleweke,” alifafanua.

“Mheshimiwa mwenyekiti kijana huyo alipokuwa amepotea mimi ndiyo nilikuwa napigiwa simu na ndugu zake na waandishi wa habari, hakupigiwa Nkamia na mtu mwingine, napigiwa mimi, mimi ndiyo mlezi wa hii sekta na mimi nilikuwa nahangaika na polisi huyu kijana kaenda wapi! Ni vitu ambavyo katika taifa hili hatujavizoea sasa huyu kijana anakuja kuniona ofisini kwangu kimekuwa kioja tena? Amekuja nimekuwa na mkutano naye for one hour ofisini kwangu lakini yule kijana ana picha tofauti na ramli zinazopigwa huko nje na humu ndani ndani ya bunge.”

“Amesema Mheshimiwa naomba aliyeniteka uchunguzi ufanyike in detail kuwa na bastola haina maana mtu atoke serikalini, bastola kila mtu anazo, alichoomba alisema tafadhali naomba uchunguzi ufanyike kwa kina mimi niliona lazima nimsindikize ni suala ambalo ni topical nchini I am the minister responsible ili kuhakikisha kwamba Watanzania wanaacha kupiga ramli, tunapata ushahidi wa kutosha ndiyo upepelezi,” alisisitiza.

BABA MWATHIRIKA WA UKIMWI AMBAKA BINTI YAKE.


ushetani, hivyo ndivyo unavyoweza kuelezea tukio la baba mzazi tena muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi kumbaka binti yake.

Kutokana na kitendo hicho, Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Musoma, Karim Mushi amemhukumu mkazi wa Kijiji cha Baranga, Wilaya ya Butiama mkoani Mara, Nyamahemba Chacha (46) kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto wake na kumsababishia maambukizi ya Ukimwi.

Akitoa hukumu hiyo juzi, Hakimu Mushi alisema Mahakama imeridhishwa pasi na shaka na ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mshtakiwa.

Akirejea ushahidi huo, Hakimu Mushi alisema Novemba 30, 2016 saa tatu usiku, mshtakiwa aliingia kwenye chumba cha watoto wake na kumuita binti yake akimweleza anaitwa na kaka yake.

Alisema baada ya mtoto huyo kutoka alimkamata na kumuingiza chumbani kwake na kumpa vitisho, alimwingilia kimwili, licha ya kutambua kuwa anaishi na VVU.



MWILI WA MWENYEKITI WA FREE MASON WAZIKWA KWA KUCHOMWA MOTO.

Marehemu Sir, Andy Chande aliyekuwa kiongozi wa Free Mason Afrika Mashariki.

Dar es Salaam. Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Freemason Afrika Mashariki, Sir Jayantilal Keshavji Chande maarufu kama Andy Chande, umeteketezwa leo Kijitonyama, jijini Dar es Salaam kupitia tukio lililodumu kwa takribani  saa moja.

Mwili huo umeteketezwa kwa moto kupitia ibaada iliyofanyika kwenye nyumba maalumu inayotumika kama sehemu ya maziko ya waumini wa dini ya Hindu.

Sir Chande alifariki dunia siku tano zilizopita wakati akipata matibabu katika hospitali ya Nairobi baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa ulitokana na matatizo ya utumbo mdogo kusambaza sumu mwilini.