Kunihusu

Picha yangu
Teacher, comedian and event master of ceremonies.

Ijumaa, 8 Juni 2018

UCHAGUZI WA UDOM WAMALIZIKA KWA AMANI.

UCHAGUZI WA UDOM WAMALIZIKA KWA AMANI.


Na Erasto Julius Ladis.

Yakiwa yamepita masaa kadha tangu majina ya washindi wa nyadhifa mbalimbali kutangazwa ilichukua takribani siku mbili kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma kuweza kupiga kura. Mchakato wa kampeni za nyadhifa mbalimbali za uongozi uliendeshwa ndani ya siku nne huku likishuhudiwa mamia ya wanafunzi waliokuwa wakijitokeza kusikiliza sera za wagombea. 
Mnamo tarehe 6 Juni 2018 ndipo zoezi la upigaji kura lilianza katika ndaki zote za elimu zinazopatikana katika chuo hiki kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki na kati. Katika ngazi ya uraisi wa shirikisho (Federal presidential) kulikuwa na wagombea wa pande mbili ambao ni Ndugu Lemma Zahir akiwa na mgombea mwenza Dada Lilian Gabriel wote kutoka ndaki ya Sayansi asilia. Mgombea mwingine alikuwa ni Ndugu Lazaro Roman na Dada Fathia Jombi kama mgombea mwenza. 
Pichani ni waliokuwa wagombea uraisi wa UDOM Ndugu Lemma Zahir na Lilian Gabriel.

Katika uchaguzi huu uliofanyika kwa haki na amani, mshindi wa ngazi ya uraisi wa federation alikuwa ni Ndugu Roman Lazaro na makamu wake Fathia Jombi ambaye alipata kura zaidi ya elfu saba akimzidi mpinzani wake kwa takribani kura 2,000.
Pichani ni mshindi wa kiti cha uraisi katika chuo Kikuu cha Dodoma 2018/2019 Ndugu Roman Lazaro na  makamu wake Dada Fathia Jombi wote kutoka COES.



TUANGAZIE UCHAGUZI WA KITIVO CHA ELIMU.

Huu ni uchaguzi ambao pia ulishuhudiwa kuwa na upinzani mkali kati ya Ndugu Shampundu Patrick aliyekuwa akichuana vikali na mpinzani wake Ndugu Kwilasa Faustine kutoka BED PPM. Baada ya uchaguzi kumalizika, matokeo yalitangazwa siku ya tarehe 8 Juni mwaka 2018 ambapo mshindi wa uraisi alikuwa ni Ndugu Shampundu Patrick akijinyakulia  akiwa na makamu wake Victoria Tembea.
Pichani ni waliokuwa waliokuwa wakiwania ngazi ya uraisi katika ndaki ya elimu (Kushoto ni mshindi Ndugu Shampundu Patrick na pembeni ni aliyekuwa akiwania tiketi hiyo pia Ndugu Kwilasa Faustine)

Wagombea wenza pia wakionesha kuwa uchaguzi haukuwa vita hapo kushoto ni Dada Zawadi na kulia ni makamu wa raisi wa COED Dada Victoria Tembea.






Raisi mteule wa KITIVO cha elimu Ndugu Patrick Shampundu.

Ijumaa, 5 Januari 2018

MWANAMKE TAMBUA NI KWANINI KILA MWANAUME HUKU TOSA BAADA YA KUFANYA NAYE MAPENZI.

Na, Erasto Ladis Julius.

Mambo vipi dada zangu? Naamini mko vizuri na mnaendelea salama na majukumu yenu ya kila siku. Wikendi ya leo ningependa nigusie kitu hiki ambacho niliwahi kukiongea kipindi cha nyuma lakini ni bora nikukumbushe uweze kujua vizuri. Kuna wakati unapata mwanaume ambaye unampenda na yeye anakupenda lakini ghafla mahusiano yanaanza kukufifia au kufa kabisa. Sasa leo nakupa sababu ujue ni kwanini hali hiyo hutokea;

1. Kutokujua chaguo lako sahihi.
Hiki ni kitu ambacho wadada wengi mnashindwa kutambua yaani unakuta dada unataka umpate mtu ambaye hakupendi aidha unampenda kwasababu ya mali au pesa alizonazo. Lakini pia unampenda mtu ambaye sio type yako mfano mtu maarufu au mtu wa muonekano mzuri  kuliko wewe. Hii itafanya daily uwe mtu wa kutokwa machozi na kuyalaumu mapenzi kumbe tatizo lipo kwako.

2. Msichana kupenda pesa, anasa au vitu vya thamani.
Kuna msemo huvuma mitaani kuwa eti mapenzi ni pesa, yawezekana kweli mapenzi yanaweza kuhusika na pesa lakini kumbuka kuwa mapenzi ya pesa hayadumu. Dada unaweza kumpenda mtu kwasababu ana pesa kumbe yeye nia yake ni kukuchezea kisha kukuacha.
 Sambamba na hilo msichana unaweza ukawa na boy ambaye anakupenda lakini pia wewe ukawa unampenda, tatizo litakuja pale wewe utakapotaka kuomba vitu vya thamani kila siku kiasi cha kumchosha hadi akakutosa.

3. Maumbile ya ndani (siri).
Binti unaweza ukawa mzuri sana kwa muonekano wa nje (physical appearance) yaani ukawa na figure nzuri, sura nzuri na kila kitu kizuri ila kuna siri moja nakwambia kuwa kama sehemu zako za siri zitakuwa pana sana basi kila boy atakuwa anachovya na kuondoka.
Utafiti unasema kuwa wanaume wengi hawapendi wanawake wenye maumbile makubwa ya siri kwani hudai kuwa hakuna ladha nzuri waipatayo. Dada ukiona kila mtu anakuacha ebu jichunguze na umuone hata daktari.

4. Tabia chafu.
Mwanzo wa mapenzi kila mtu huficha makucha kutokuonesha tabia zake lakini mambo huja kuwa tofauti pale ambapo mtazoeana. Utakuta msichana ni mpenda wanaume au kwa lugha ya kawaida niseme ni malaya. Tambua kuwa mapenzi ni kuheshimiana na mapenzi yana wivu sana kwa hyo ukiwa ni kiruka njia hakuna mwanaume mwenye moyo wa chuma wa kukuvumilia.
Tabia zingine chafu ni kama kutokuwa na lugha nzuri, kutokuvaa mavazi ya staha na kutokuwa na heshima.

5. Makundi au marafiki.
Kuna wakati boy akawa anakupenda sana lakini kwasababu ya marafiki au makundi mabaya uliyonayo yakamtia wasiwasi bwana wako. Yawezekana boy wako hapendi unywe pombe ila akaona una kundi la wanywa pombe pia boy wako akaona una kundi la watumiaji ambao yeye hawaamini basi tegemea kuachwa.
Kumbuka kuwa marafiki wanaweza kuharibu hata uhusiano wako aidha kwa kukupa maneno ya ajabu kuhusu boy wako au kumtongoza kabisa ili wajue umempendea nini.

6. Wivu na kelele za mara kwa mara.
Mapenzi ya kweli yana wivu lakini wivu ulivuka mipaka huwa ni kero. Wanaume wengi hawapendi kabisa kelele za mara kwa mara na badala yake hupenda mapenzi ya utulivu yenye amani tele. Sio mwanamke kila wakati mara ushike simu ya mwenza wako mara ukiona kasimama na msichana unune, aisee utaambulia mabua.

7. Maringo na usumbufu ukitongozwa.
Kuna wakati mtu akakupenda na kuamua kukufuata ila ukawa una ringa na kumkataa. Mtu huyo huendelea kukomaa na wewe hata baada ya miezi 6 mwisho anakata tamaa sasa siku ukimkubalia na kumvulia nguo hufanya kisha kukutosa. Hii ni kwasababu unakuta umemkubalia muda ambao yeye hakupendi na amekata tamaa na wewe.


8. Hulka ya wavulana wenyewe.
Ukweli kuna wavulana wengine ambao tayari walishakuwa play boys ambao hutamani kila sketi isiwapite. Aina hii ya wanaume huwa na maneno matamu sana na huwa na mbinu nyingi kuwashawishi akina dada na kwasababu akina dada pia ni dhaifu basi hukubali na kuambulia maumivu.
Dada zangu kuna mambo mengi sana ambayo yanafanya uachwe lakini hayo yanakutosha kwa hiyo wajibu ni wako kujipanga kuwania mama bora ila sio kufanywa choo cha kanisa eti kila muumini anaingia.
Mwanamke uchi wako una thamani kubwa zaidi ya elfu 50 ambayo utapewa siku moja. Mwili wako ni lulu ya kuringia kwa watu, kwa hiyo jitambue. Mwili wako ni zaidi ya gari au nyumba kisha uumizwe moyo.


Toa maoni hapa 

Jumanne, 2 Januari 2018

 MAAJABU YA WALEVI NCHINI  NEWZEALAND.


Kutokanana marufuku dhidi ya unywaji pombe hadharani wakati wa sherehe za mwaka mpya nchini New Zealand kikundi kimoja cha watu kutoka eneo la kisiwa cha Coromandel nchini humo kimeshangaza watu baada ya kutengeneza kisiwa kidogo cha udongo kisiwani hapo ili wanywe pombe bila kukamatwa na polisi kwa kukiuka marufuku hiyo.
Kwa mujibu wakazi hao, walitengeneza kisiwa hicho wakati maji yamekupwa ili wanywe pombe kwa uhuru kutokana na kwamba hilo ni eneo la bahari la kimataifa ambalo halimilikiwi na taifa lolote hivyo wasingekamatwa na vyombo  vya dola.
Kamanda wa Polisi wa eneo hilo Inspekta John Kelly alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema huo ni ubunifu wa hali ya juu sana na laiti kama angelelijua suala hilo mapema angeungana nao.

MATUKIO MBALIMBALI YALIYOJITOKEZA KWENYE BIRTHDAY YA ERASTO THE NINJA TAREHE 1 JANUARI.


Ni baada ya kumwagiwa maji na marafiki.

Maji hayakuwa ya dunia hii

Class mate pia walikuwepo

Raia wengine hawakucheza mbali

Baadhi ya wasanii wa UDOM wakiongozwa na Mhayudi wa kwanza kushoto.

Ilikuwa ni picha ya mwaka.


Asante sana kwa support yenu wadau wangu wa nguvu.



Ijumaa, 29 Desemba 2017

LISTI YA WASANII 10 WALIOFANYA VIZURI MWAKA 2017

HII NI LISTI YA WASANII 10 KUTOKA TANZANIA WALIOFANYA POA SANA MWAKA 2017.

Na, Erasto The Ninja.

Yakiwa yamesalia masaa machache sana kuweza kuukamilisha mwaka huu basi ingekuwa ni vizuri zaidi kama ningetaja wasanii 10 bora ambao wameweza kufanya poa sana mwaka 2017. Karibu twende pamoja.

1. ASLAY
Akiwa ni moja kati ya vijana waliotoka kupitia mgongo wa lebel ya Mkubwa na Wanawe kutoka Temeke basi Aslay amekuwa ni moja kati ya vijana ambao wamefanya poa sana mwaka huu. Hakuna wa kupinga kuwa kona zote za mitaa ya hapa nchni Tanzania ulikuwa huwezi kupita bila kusikia wimbo wa Aslay ukichezwa. Akiwa amefanya kazi zake kwa Shirko producer wa Moja Moja Records lakini pia Aslay alifanya hit kali pia kutoka kwa producer Zest. Nyimbo zake kali alizotoa mwaka huu ni kama Natamba, Baby, Pusha na nyimbo kibao tu ambazo siwezi kuzitaja zote.

2. NANDY.
Ni product kutoka Tanzania House of Talent ambapo baadhi ya wasanii kama Barnaba, Amin, Rachel, Beka na Lameck Dotto walipitia hapo. Kuna watu husema kuwa Nandy ndio amekuwa mrithi wa Ruby hasa kwa nyimbo zake kali na jinsi anavyoweza kutumia sauti yake vizuri. Nandy ndiye msanii wa kike ambaye kwa mtazamo wangu ndio kafanya vizuri zaidi mwaka huu.

3. DIAMOND PLATNUMZ.
Kiuhalisia mimi ni Team Kiba ila kwenye kitu kizuri siwezi kusema uongo. Diamond kafanya vizuri sana kwa hit zake alizotoa mwaka huu akiwa pamoja na team yake ya WCB. Diamond amefanya kazi na wasanii wakubwa kama Morgan, Patoranking na  The Big Boss *Rick Ross* kutoka USA. Chini ya Producer Laizer jua kuwa Diamond kafanya ngoma kali kama Sikomi, Love you die na ngoma kibao zingine.

4. ALI  KIBA.
Ni kijana kutoka Kariakoo Dar es Salaam aliyekuja kutambulika zaidi mwaka 2007 na wimbo wake wa Cinderella aliofanya pale *G. Record* chini ya producer *KGT*. Japo hakuwa na nyimbo nyingi ila hakuna wa kubisha kuwa "Seduce Me" no wimbo wa Kiba ambao ulikuwa gumzo sana nchini Tanzania hasa baada ya kuvunja record ya Vevo Afrika Mashariki. Ali Kiba amepata shoo nyingi sana hasa baada ya kutoa wimbo wa Seduce me uliofanyika kwenye studio za Man Walter (Combination Sound).

5. WEUSI.
Nashindwa nimtaje nani aingie kwenye list hii ila kwasababu wote hufanya kazi kwa ushirikiano basi sina budi kuwaweka hapa. Sio Joh Makini, G. Nako wala Nikki wa Pili ambaye unaweza kutia shaka kwenye kazi aliyoifanya kwenye tasnia ya muziki mwaka huu. 

6. VANESSA MDEE.
Moja kati ya wadau ambao husemekana kuwa wana uwezo mkubwa sana wa kutema kimombo basi Vanessa kafanya vizuri sana mwaka huu. Moja kati ya nyimbo alizotoa ni "Mapenzi ya Kisela" akiwa na "Mr. P" wa kundi la "P-Square" kutoka Nigeria. Vanessa Mdee pia kafanya collabo kibao za kimataifa na ndani ya bongo.

7. ZAIID.
Hakuna ngoma iliyopata gumzo bongo kama ngoma ya Zaiid "Wowowo" ambayo imefanya poa sana kwenye vituo vya radio na Tv hapa nchini Tanzania. Zaiid alikuwa kama ni msanii mpya kwenye game la muziki hasa kwa baadhi ya watu lakini ukweli ni kwamba Zaiid ni msanii ambaye alikuwa na nyimbo nyingi tu hata kabla ya wimbo wa  "Wowowo".

8. ROSTAM.
Ni kundi ambalo lilianza kama mzaha ila mwisho likawa official. Roma Mkatoliki kutoka Tanga na  Stamina kutoka Morogoro ni vijana wawili walioweza kufanya poa sana hasa na wimbo wao wa Hivi ama vile na Kibamia zilizofanyika pale Kiri Record kwa Producer Don.

9. ______________

10. _____________

Nimeacha wazi hapo namba 9 na 10 ili nawewe uweke wasanii wako wawili kukamilisha list hiyo.

Jumanne, 12 Septemba 2017

TUJIKUMBUSHE KIDOGO JUU 2PAC.


Leo Septemba 13 ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha aliyewahi   kuwa nyota mkubwa sana kwenye miondoko ya Hip Hop namzungumzia 2pac Shakur a.k.a Makaveli. Ni msanii aliyezaliwa mwaka 1971 East Harlen-New York nchini Marekani na alianza kazi ya muziki mwaka 1987 akiwa kwenye kundi la Digital Underground. 
Mbali na kuwa mwanamuziki 2Pac alikuwa ni muigizaji na aliwahi kucheza muvi 6 akiwa kama starring na moja kati ya filamu aliyowahi kutoa ni Gang Related ya mwaka 1993. Hadi mauti yanamkuta 2Pac Shakur alikuwa amewekeza vizuri kwenye albamu maana aliacha albamu 5. Moja kati ya albamu zake ni All eyes on me, Strictly 4 Maniggaz na 7 Day theory (Don Kiluminant).

2Pac Shakur aliwahi kushirikiana na wasanii kama Nate Dogg, Snoop Dog, Rich Richie na The Notorious B.I.G. Amewahi kuwa kwenye kundi la Thug Life na lebo ya Interscope mwaka 1991-1995 kisha lebo ya Death Row mwaka 1995-1996.

2Pac  Shakur alifariki dunia majira ya saa 10 jioni Septemba 13 mwaka 1996 ikiwa ni siku 6 tangu kutokea kwa shambulizi lake. Usiku wa tarehe 7 septemba 1996 wakati Pac akitokea kwenye mpambano wa masumbwi kati ya rafiki yake Mike Tyson dhidi ya Bruce Ledon kwenye barabara ya Flamingo ndipo alipovamiwa na watu wasiojulikana wakiwa kwenye gari na kufanikiwa kumchapa risasi 4 na moja kati hizo risasi ilipiga pafu lake la kulia. Baada ya shambulio hilo  2Pac Shakur alikimbizwa kwenye hospitali ya University Medical Centre of Sourthen Nevada ambako ndiko mauti yalimkuta. Mtu aliyefanya shambulio lile hakuwahi kujulikana hadi leo japo kuna watu wengi sana walihusishwa na tukio hilo kama vile hasimu wake wa wakati huo B.I.G na Anderson.

Tutamkumbuka sana 2Pac Shakur kwa uwezo wake mkubwa wa kufanya muziki wa Hip Hop. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu 2Pac mahali pema peponi, Amina.

Imeletwa kwenu na Erasto The Ninja
Tel: 0768801115

Jumatano, 7 Juni 2017

KUWA WA KWANZA KUPATA TAARIFA NA BURUDANI KUPITIA BLOG HII.

Sasa ninjamedialive itakuwa ikikupa taarifa mbalimbali za burudani, siasa, uchumi na jamii popote pale ulipo. Tafadhali tembelea ukurasa huu ili uwe unapata taarifa zote uzipendazo.

 

MJANJA HAPITWI NA KITU.